Thursday, April 14, 2016

Walio ‘benchi’ kusubiri kazi mpya waongezeka

,
;

Walio ‘benchi’ kusubiri kazi mpya waongezeka



By Fidelis Butahe, Mwananchi fbutahe@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Uamuzi wa kutengua uteuzi wa makatibu wakuu, wakuu wa mikoa, wilaya na watumishi wengine waandamizi kwa maelezo kuwa watapangiwa kazi nyingine, inazidi kuongezeka baada ya Rais kumvua Anne Kilango ukuu wa mkoa na kuahidi kumpangia kazi nyingine.
Mpaka kufikia jana, makatibu wakuu sita na wakuu wa mikoa na wilaya kumi walikuwa wamevuliwa nyadhifa zao na kuelezwa na mamlaka zao za uteuzi kuwa watapangiwa kazi nyingine huku nafasi zao wakipewa watu wengine.
Utenguaji wa uteuzi wa makatibu wakuu sita na mkuu mmoja wa mkoa umefanywa na Rais John Magufuli tangu alipoingia madarakani Novemba 5, mwaka jana huku Jakaya Kikwete, aliyeongoza Serikali ya Awamu ya Nne, akitengua uteuzi wa wakuu tisa wa wilaya na mikoa ambao mpaka sasa hawajapangiwa kazi nyingine.
Kitendo cha kuwaweka pembeni wateule hao wa Rais kimezua maswali mengi, ikiwa ni pamoja na utaratibu wa ulipwaji wa stahiki mishahara na posho mbalimbali hasa kwa wale wanaokaa muda mrefu bila kupangiwa kazi nyingine.
Baadhi ya wachambuzi waliozungumzia suala hilo walisema licha ya mamlaka ya uteuzi ya watumishi hao kuwa chini ya rais, hoja ya kupangiwa majukumu mengine haraka kwa lengo la kuokoa fedha haikwepeki.
Kwa mujibu kwa kifungu cha 13 (6) cha Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2014, mtumishi wa umma wa ngazi ya uteuzi wa Rais, akivuliwa wadhifa, mshahara wake wa mwezi utabaki kama ulivyo isipokuwa posho aliyokuwa akipokea wakati wa uteuzi itapangwa kulingana na matoleo ya ofisi kuu ya Utumishi wa Umma.
Pia kifungu cha 20 (1) cha kanuni hizo kinasema: “Iwapo mtumishi wa ngazi ya uteuzi wa Rais, atakuwa hayupo katika nafasi yake ya utumishi, nafasi yake itashikiliwa na mtumishi mwenye wadhifa sawa na wake au anayemfuatia kwa idhini ya Katibu Mkuu au mkuu wa taasisi au Katibu Mkuu Kiongozi kulingana na wadhifa wa anayeondoka.”
Hata hivyo, makatibu wakuu walioondolewa nafasi zao zilijazwa na wengine walioteuliwa na Rais Magufuli, huku wakuu wa wilaya na mikoa pia nafasi zao zikijazwa na wengine na hivyo kuwafanya wote kuendelea kusubiri majukumu mengine.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Angela Kairuki, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, hakutaka kuzungumzia suala hilo.
“Mkuu wa utumishi wa umma ni Katibu Mkuu Kiongozi. Yeye ndiye atakuwa na nafasi nzuri ya kusema hilo, maana mimi nikisema nitakuwa kama naingilia.”
Jitihada za kumpata Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi hazikufanikiwa baada ya kutafutwa kwa wiki mbili mfululizo bila kupatikana.
Katibu mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi (Tucta), Nicolaus Mgaya alisema ni jambo linaloweza kuzua mjadala iwapo watumishi hao watakaa muda mrefu bila kupangiwa majukumu mengine.
“Kwanza wanalipwa fedha za umma bila kuwajibika popote. Ni vyema uteuzi wa mtu ukitenguliwa isichukue muda mrefu awe amepangiwa majukumu mengine,” alisema Mgaya.
“Inawezekana mtu akalipwa mpaka siku anastaafu akifikisha miaka 60. Na ikitokea hivyo na pia kama rais hajamstaafisha mtu huyo ana haki pia ya kulipwa na ataendelea kulipwa tu.”
Alisema litakuwa jambo jema kama uteuzi mpya utafanyika haraka iwezekanavyo ili kuondoa sintofahamu iliyopo sasa kwa kuwa jambo hilo lisipotazamwa kwa kina, nchi itajikuta inawalipa mishahara watumishi wanaosubiri kupangiwa kazi nyingine.
Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu Ruaha, Profesa Gaudence Mpangala aliungana na Mgaya na kufafanua kuwa jambo hilo si sawa na linahitaji kukumbushwa mara kwa mara.
Alisema ili kuondokana na suala hilo, inapaswa watendaji hao kupangiwa majukumu mengine muda mfupi baada ya kuwekwa kando.
“Ninachokiona ni kama kila Serikali kutaka kuwa na watu wapya. Rais Magufuli ameingia madarakani na inaonekana wazi kuwa anataka kufanya kazi na watu wapya. Tazama makatibu wakuu waliowateua hivi karibuni na hata kitendo cha kumuondoa Sefue,” alisema Mpangala.
Utenguaji wa uteuzi
Tangu aingie madarakani, Rais Magufuli amekuwa akisimamisha, kutengua uteuzi na kutimua watumishi kadhaa waandamizi na kati ya aliotengua uteuzi wao, alisema kuwa atawapangia kazi nyingine.
Desemba 30, mwaka jana Rais Magufuli alifanya uteuzi wa makatibu wakuu na naibu 50 wa wizara, huku akiwaacha baadhi yao ambao alisema watapangiwa kazi nyingine.
Walioachwa ni pamoja na Dk Donnan Mmbando (Afya), Balozi Liberata Mulamula (Mambo ya Nje), Omari Chambo (Nishati na Madini), Jumanne Sagini (Tamisemi) na Joyce Mapunjo (Afrika Mashariki).
Katika orodha hiyo, yupo Balozi Ombeni Sefue, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, ambaye alikuwa mteule wa kwanza wa Rais Magufuli kuondolewa Ikulu akimpisha Balozi John Kijazi.
Rais alisema atampangia kazi nyingine Balozi Sefue, lakini hadi sasa bado haijatangazwa kazi aliyopangiwa.
Wengine ambao uteuzi wao ulitenguliwa ni aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Dk Shaban Mwinjaka kupisha uchunguzi baada ya kutajwa kuhusika katika matumizi mabaya ya Sh13 bilioni kwenye Shirika la Reli Tanzania (TRL).
Mwinjaka alikuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi ya Katibu Mkuu kuondolewa na Rais Magufuli. Uteuzi wake ulitenguliwa wakati Dk Magufuli alipotimiza mwezi mmoja tangu awe Rais wa Awamu ya Tano.
Mbali na Rais Magufuli kuwaweka pembeni watumishi hao, Kikwete naye aliwaweka pembeni watumishi kadhaa kwa sababu tofauti.
Desemba 7, 2014 Kikwete aliteua wakuu wapya wa mikoa, akiwapandisha cheo wakuu wa wilaya na kuwaacha watatu akieleza kuwa watapangiwa kazi nyingine.
Walioachwa kwa ahadi ya kupangiwa kazi nyingine ni Dk Christine Ishengoma (Iringa) na Kanali Fabian Massawe (Kagera). Katika panga hilo pia alikuwepo Kanali Joseph Simbakalia aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Mtwara, ambaye tayari ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzi ya Nje (EPZA).
Pia Februari 19, 2015 Kikwete alihitimisha uteuzi wa nafasi za kisiasa za mkupuo kwa kuwang’oa wakuu wa wilaya 19, kuteua wapya 27, kuhamisha 64 na 42 wakibaki kwenye vituo vyao.
Katika kundi la wakuu wa wilaya 19 waliong’olewa, uteuzi wa wakuu 12 ulitenguliwa na saba ilielezwa kuwa watasubiri majukumu mapya.
Wakuu saba wa wilaya waliobadilishiwa majukumu ni Brigedia Jenerali Cosmas Kayombo, aliyekuwa Simanjiro, Kanali Ngemela Lubinga (Mlele), Juma Madaha (Ludewa), Mercy Silla (Mkuranga), Ahmed Kipozi (Bagamoyo) na Elinas Pallangyo (Rombo).     
Read more →

VIONGOZI WA VIKOSI KAZI VYA NGOME ZA CHAMA TAIFA

,
;
ACT Wazalendo


VIONGOZI WA VIKOSI KAZI VYA NGOME ZA CHAMA TAIFA

Katika vikao vyake vya kwanza vilivyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 09/04/2015, Wajumbe wa Vikosi Kazi (Task Forces) vya Ngome za Chama cha ACT Wazalendo wamechagua viongozi wake wakuu. 
Viongozi waliochaguliwa ni Waratibu na Manaibu wao kama ifuatavyo:
NGOME YA WAZEE 
Mratibu Taifa:
Ndugu Hamis Hassan Makapa
Naibu Mratibu Bara
Ndugu Wilson Mushumbusi
Naibu Mratibu Zanzibar
Ndugu Abdallah Omar Abdallah
NGOME YA WANAWAKE
Mratibu Taifa
Ndugu Chiku Abwao
Naibu Mratibu Bara
Ndugu Easther Kyamba
Naibu Mratibu Zanzibar
Ndugu Nawiye Abdallah Mussa
NGOME YA VIJANA
Mratibu Taifa
Ndugu Ricapo Bakari
Naibu Mratibu Bara
Ndugu Edna Sunga
Naibu Mratibu Zanzibar
Ndugu Haji Usi Haji
Mohammed Massaga,
Katibu, Kamati ya Mafunzo na Uchaguzi
Read more →

Woman accused of live-streaming rape on Periscope

,
;

Woman accused of live-streaming rape on Periscope

AccusedImage copyrightAP
Image captionMarina Lonina is accused of filming her boyfriend Raymond Gates sexually assaulting a teenager
A woman from Ohio has been charged with streaming the rape of a teenage girl via Twitter's live video app Periscope.
The offence is alleged to have occurred two months ago and was brought to the authorities' attention by someone who said they had seen the broadcast.
The accused's lawyer says that she "categorically" denies the charges.
An expert said the case highlighted the impossibility of controlling content on live-streaming services, which are gaining in popularity.
According to the indictment, the sexual assault took place in the city of Columbus on 27 February.
Marina Lonina is also accused of taking a photo of the 17-year-old in a state of undress the previous night.
Lonina's boyfriend, Raymond Gates, has been accused of carrying out the assault. It is not yet known how he intends to plead.
PeriscopeImage copyrightPeriscope
Image captionPeriscope attracted more than 10 million users within a year of being launched
The two face charges of rape, kidnapping, sexual battery and pandering sexually-oriented matter involving a minor.

Inaccurate systems

Twitter could not be reached for comment.
But this is not the first time Periscope has been linked to an alleged offence.
Earlier this month, it was reported that police in London had intervened after a fight between two rival gangs had been arranged via the app.
Other incidents include:
The app has hosted more than 100 million broadcasts since it launched last year, the vast majority of which are innocuous.
But the issue of live-streamed crime could become more common as the activity becomes more mainstream.
FacebookImage copyrightFacbook
Image captionFacebook announced on Tuesday that it is giving more prominence to live video streams
Earlier this week, Facebook announced it was adding a tab to its app to help users find live-streamed videos.
The social network had already altered the algorithm of its news feeds to prioritise such feeds.
"The volume of content being created and uploaded every day is far too great to be regulated manually and automatic systems are simply too inaccurate to be practical," commented Dr Joss Wright from the Oxford Internet Institute.
"There is almost no practical way to prevent content like this being uploaded and shared if people want to do it and any system to do so would also have serious implications for freedom of expression and the publication of legitimate but controversial content.
"The internet has undoubtedly made this case worse for the alleged victim. But as with other real-world crimes, prevention is not always possible."
Read more →

Tanzania kuendelea kunufaika na miradi ya Marekani

,
;

Tanzania kuendelea kunufaika na miradi ya Marekani


Waziri wa Mambo ya Nje,Afrika Mashariki,Kikanda
Waziri wa Mambo ya Nje,Afrika Mashariki,Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa Dr Augustine Mahiga  
By Vicky Kimaro na Suzan Shao, Mwananchi
Dar es Salaam.  Wakati misaada ya Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC), ikisitishwa, Marekani imeihakikishia Tanzania bado itaendelea kupata Dola 700 milioni ambazo ni sawa na Sh152 trilioni  katika kufadhili miradi ya afya na elimu.
Katika Kikao cha  Waziri wa Mambo ya Nje,Afrika Mashariki,Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa Dr Augustine Mahiga na Balozi wa Marekani nchini Mark Childress  kilichofanyika juzi, lengo lilikuwa ni Tanzania kutaka kuhakikishiwa iwapo miradi inayofadhiliwa na Marekani nchini kama bado nchi hiyo itaendelea kuifadhili ama  itasitishwa.
Hata hivyo, Balozi huyo wa Mareani nchini alimuhakikishia Waziri Mahiga kuwa licha ya changamoto  mbali mbali za kisiasa zilizopo nchini, bado nchi yake imeona umuhimu wa  kuendeleza  mahusiano katika kutoa misaada ya maendeleoa hasa katika sekta ya elimu na afya
Read more →

JPM apekua mafaili ya CAG wa Kikwete

,
;

JPM apekua mafaili ya CAG wa Kikwete



By Mwandishi Wetu, Mwananchi mwananchipapers@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Kilio cha muda mrefu cha wabunge na ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kimesikika.
Kilio hicho kilikuwa ni kufanyia kazi taarifa na mapendekezo mbalimbali dhidi ya ufisadi, usimamizi mbovu, ukiukwaji kanuni na malipo ya wafanyakazi hewa, lakini hakikuwa kikifanyiwa kazi hadi baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani.
Rais John Magufuli sasa ameanza kupekua mafaili aliyoyakuta mezani yanayofichua ufisadi na kupendekeza njia bora ya kudhibiti, akifanyia kazi kwa kutumbua majipu na kuweka kwenye mkakati mapendekezo hayo, hasa yaliyotolewa na CAG.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini hatua zilizochukuliwa na Serikali ya JPM ni matokeo ya kufanyia kazi mapendekezo yaliyomo katika ripoti za CAG za kuanzia mwaka 2009/ 2010 na 2013/ 2014 ambazo zilitolewa wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne.
Ripoti hizo zinapendekeza namna bora ya kuongeza vyanzo vya mapato pamoja, kudhibiti na kuratibu matumizi ya fedha, likiwamo suala la upunguzaji wa mishahara ambalo limeibua mjadala tangu Rais Magufuli alipolitamka wakati akiwa mapumzikoni Chato mkoani Geita.
Ripoti hizo zilikuwa zikifanyiwa kazi nusunusu au kwa shinikizo la Bunge la Jamhuri ya Muungano, kiasi cha CAG kuonekana kama anakata tamaa.
“Ninapenda kuifahamisha Serikali kwamba, mapendekezo ninayoyatoa mara kwa mara yana lengo la kuhakikisha kunakuwa na hatua madhubuti na umakini katika kuimarisha ukusanyaji na utumiaji wa mapato na rasilimali za Taifa,” anasema CAGk katika ripoti ya mwaka 2013/ 2014.
“Mapendekezo hayo pia yanalenga kuhakikisha matumizi ya fedha za umma yanaidhinishwa na wenye mamlaka na fedha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Kwa hali hiyo, kwa kuzingatia sheria na kanuni katika kutumia rasilimali za Taifa; thamani ya fedha, tija na ufanisi vyaweza kufikiwa.
“Kwa misingi hiyo, ninaona ni vyema kuyarudia tena mapendekezo niliyoyatoa katika ripoti zilizopita ambayo hayajatekelezwa au yametekelezwa kwa kiwango kidogo na Serikali, Bunge, bodi za wakurugenzi na watendaji wakuu wa mashirika ya umma.”
Baadhi ya mapendekezo ya CAG ambayo hayakuwahi kufanyiwa kazi ni kuweka usawa katika marupurupu yatolewayo na mashirika na taasisi nyingine za umma, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kutumia mita za kupima mafuta zilizotelekezwa, kufuatilia misamaha ya kodi, pamoja na kuhimiza matumizi ya mashine za elektroniki.
Mapendekezo hayo na mengine mengi yamefanyiwa kazi kikamilifu na Serikali ya JPM katika kipindi kifupi na kufanikiwa kuokoa mabilioni ya fedha.
Ripoti ya mwaka 2009/ 2010 na hata ya mwaka 2013/ 2014, inaonyesha CAG alipendekeza uwepo usawa katika marupurupu yatolewayo na mashirika na taasisi nyingine za umma.
“Kuna umuhimu kwa Serikali kuhakikisha kuwa kuna uwiano katika marupurupu wanayopata menejimenti na bodi za wakurugenzi wa mashirika na taasisi nyinginezo za umma, kutokana na ukweli kwamba rasilimali wanazotumia (kama posho za vikao, ada za bodi za wakurugenzi) ni rasilimali za Umma. Hii itasaidia kuondoa tofauti zilizopo sasa, kuongeza ufanisi na uwajibikaji katika mashirika na taasisi nyingine za umma,” alisema.
Pendekezo hilo halikufanyiwa kazi, lakini hivi karibuni Rais Magufuli akiwa Chato, Geita alitangaza kurekebisha mishahara ya wafanyakazi, akisema atapunguza mishahara ya wakurugenzi wa taasisi za umma wanaolipwa hadi Sh40 milioni.
“Katika Serikali ninayoongoza, sitegemei kumlipa mtumishi zaidi ya Sh15 milioni. Tayari nimeunda tume kushughulikia hilo,” alisema Rais Magufuli ambaye amejikita katika kusimamia makusanyo ya mapato, huku akidhibiti matumizi na kupambana na wezi wa mali ya umma.
Katika ripoti ya mwaka 2012/2013, CAG alishauri mita za kupima mafuta zilizofungwa na TPA zianze kufanya kazi ili upimaji mafuta yanayoingia nchini ufanywe kwa usahihi.
“Mita hizo ziliwekwa tayari kwa matumizi kwenye bandari za Tanga na Dar es Salaam kwa ajili ya kusaidia kudhibiti mapato yanayopotea kutokana na kutokuwa na vifaa vizuri vya kupimia shehena za mafuta zinazoingia nchini… Hata hivyo, mita hizo zimetelekezwa kwa miaka kadhaa sasa,” anasema CAG.
CAG alisikitishwa na hali hiyo kwa sababu kutotumia vipimo hivyo sahihi na badala yake kupima kwa kutumia kijiti, kulisababisha upotevu wa mapato ya Serikali.
Lakini Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo alidai vifaa hivyo havikidhi viwango vinavyotakiwa.
“Baada ya matatizo hayo kushindikana, mamlaka ikaamua kuendelea kutumia njia zisizo za kielektroniki (fimbo ya kutumbukiza kwenye matangi ya mafuta) kwenye kupima shehena za mafuta yanayoingia nchini. Kitendo hicho kina athari kwa mapato ya Mamlaka ya Mapato Tanzania katika uhakiki wa usahihi wa kiasi cha kodi kinacholipwa kutokana na upimaji wa shehena hizo za mafuta bila ya kutumia vifaa stahiki na athari katika uendeshaji wa shughuli za TPA,” alisema.
Februari 11, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitembelea eneo la Kigamboni kukagua ujenzi wa mita hizo kwa ajili ya kupima mafuta yanayoingia ili kujua usahihi wa kiasi cha mafuta yaliyoingia.
Mapendekezo mengine yaliyowahi kutolewa na hayakufanyiwa kazi katika kipindi chote cha utawala wa Rais Kikwete ni kudhibiti misamaha ya kodi.
“Ninapendekeza Serikali iimarishe mfumo wa udhibiti na usimamizi wa misamaha ya kodi inayotolewa na menejimenti ya TRA (Mamlaka ya Kodi Tanzania) iimarishe mfumo wa ukaguzi na uchunguzi kupunguza migogoro kuhusiana na ulipaji wa kodi,” alisema.
“Pia, kuwe na kikao cha kimkakati kujadili maeneo maalumu na njia za kukuza ukusanyaji wa mapato pamoja na kushughulikia rufaa za kesi za kodi nchini. Mamlaka ya Mapato Tanzania kutoza wafanyabiashara wasiotumia mashine za kielektroniki. Serikali itoe miongozo kwa taasisi zake kuacha kufanya biashara na wazabuni wasiotoa risiti za kielektroniki.”
Katika kipindi chote cha kampeni za urais Magufuli aliahidi kufuta misamaha yote ya kodi isiyo na tija, na baada ya kuingia madarakani siyo tu alitimiza ahadi yake kwa Serikali yake ilianza kufuatilia wote waliotumia vibaya misamaha yakiwamo mashirika ya dini.
Kuhusu ukwepaji kodi Novemba 27 2015 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alifanya ziara ya kushtukiza TPA ambako ilibainika makontena 349 yamepotea, na siku tano baadaye yaani Desemba 3, 2015 Majaliwa alifanya ziara ya pili ambako alitaja makontena 2431 yaliyopitishwa bila kulipiwa kodi kati ya Machi na Septemba 2014. Serikali iliwataka wahusika wote kulipa kodi huku ikiwasimamisha au kuwafukuza wafanyakazi waliohusika.
Hata suala la kuwaondoa wafanyakazi hewa kutoka kwenye daftari la malipo ni ushauri wa CAG.
“Kuhusu usimamizi wa rasilimali watu na taarifa za mishahara, Serikali inashauriwa kuhakikisha kuwa kasoro hii haitokei na maafisa masuuli wote kuhakikisha mishahara iliyolipwa kwa wasio watumishi wa umma inarudishwa kutoka kwa watumishi hao na kuwasilishwa Hazina,” anasema.
Machi 2016 Rais Magufuli alipowateua wakuu wa mikoa na kuwaapisha aliwaagiza kufanya kazi ya kuwaondoa wafanyakazi hewa wote na kuonyesha hakuwa anatania, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela aliyedai hakukuwa na wafanyakazi hewa wakati wapo amefukuzwa kazi.
CAG alipendekeza pia maafisa waliostaafu katika balozi za Tanzania warudishwe nyumbani na nafasi zao kujazwa mara moja. Utekelezaji ulifanyika Januari na Machi wakati balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Radhia Msuya, pamoja na watumishi wengine watano, waliporejeshwa nchini.
Wengine ni Balozi wa Tanzania aliyeko London, Uingereza, Peter Kallaghe, Balozi wa Tanzania nchini Italia, Dk James Msekela; na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan, Dk Batilda Buriani, baada ya mikataba yao kumalizika.
Wanasiasa walioongea na Mwananchi walipongeza hatua za Rais, lakini baadhi wakata kuwepo na mfumo wa kufanya uamuzi kama huo.
“Rais Magufuli anastahili pongezi kwa hatua alizozichukua kwa kuwa hazikufanywa na mtangulizi wake,” alisema mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini.
“Kuna vitu vingi vinavyoainishwa ndani ya ripoti za CAG na mojawapo ni Sheria ya Manunuzi ya Umma. Hii imeelezwa mara nyingi kuwa inachangia upotevu wa fedha za Serikali kwa kiasi kikubwa. Kinachotakiwa iondolewe au ifanyiwe marekebisho ili kukabiliana na watu wanaouza bidhaa au huduma zao kwa bei ya juu kuliko ya soko.”
Alisema nia nzuri ya Rais kukabiliana na rushwa pamoja na ufisadi itakuwa endelevu endapo kila mtu ataipa kipaumbele wakiwamo wasaidizi wake, lakini akaongeza kuwa jambo hilo linawezekana endapo kutakuwa na kanuni zinazombana kila mtumishi wa umma.
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema: “Kama ni ufuatiliaji ni jambo zuri, na mfano mzuri ni hili la watumishi hewa. Tunachotaka kukiona hivi sasa ni hao wanaofanya mpango wa malipo hayo kuchukuliwa hatua.”
Mchungaji Msigwa alisema wapinzani watapata nafasi ya kuzungumzia ufuatiliaji huo wa Rais Magufuli pale watakapoona kuwa wahusika wote wanachukuliwa hatua, akidai sasa kuna maneno mengi kuliko vitendo.
“Mbona hatujaona wakurugenzi wa halmashauri wakichukuliwa hatua maana wao wanajua siri ya mishahara hewa,” alisema.
Kwa upande wake, mbunge wa Gairo (CCM), Ahmed Shabiby alisema ofisi ya CAG ni chombo cha Serikali na kinafanya kazi kwa mujibu wa sheria hivyo ni lazima ripoti zake zitekelezwe kwa ajili ya maslahi ya nchi.
“Utekelezaji wa ripoti ya CAG unaipa nguvu ofisi yake lakini pia nashangaa kwa nini mapendekezo yake yalikuwa hayatekelezwi miaka ya nyuma?”
Mbunge wa Manyovu (CCM), Albert Obama alisema kila zama zina njia zake za kufuatilia masuala muhimu licha ya kasi ya ufuatiliaji ya Serikali iliyopita ilikuwa ndogo.
“Rais anataka kuleta nidhamu mpya ndani ya nchi kwa kupambana na masuala ya rushwa na ufisadi,” alisema Obama ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji (PIC).
“Nadhani huu ni wakati wa kumpa Rais ushirikiano ili kuweza kubainisha masuala mbalimbali. Hizi ni zama za wanyonge kunufaika na nchi yao.”     
Read more →

South Africa's runaway lion Sylvester given own pride

,
;

South Africa's runaway lion Sylvester given own pride

  • 13 April 2016
  •  
  • From the sectionAfrica
Sylvester the lionImage copyrightSAN Parks
Image captionIt is thought Sylvester the lion was running away from older male lions when he got through the fence at Karoo National Park
A South African lion called Sylvester who twice fled a national park will be rehoused rather than put down, and encouraged to become an alpha male.
Karoo national park authorities had originally considered putting Sylvester down but will now rehouse the animal away from male competition.
The lion's plight was highlighted in a Twitter campaign in South Africa.
Sylvester will now join two young female lions in Addo Elephant National Park in the Eastern Cape province.
Sylvester escaped at the end of March by crawling under an electric fence after heavy rain dislodged earth, a park spokesperson said at the time.
It is thought three-year-old Sylvester was running away from threatening older males.
The move will establish him as the dominant male, said Fundisile Mketeni, CEO of South Africa National Parks.
"There is always a risk that this lion may break out again but this will be mitigated to a large extent by reducing any potential conflict with other males," Mr Mketeni added.
Last June, Sylvester went on a three-week sheep-killing spree, wandering 300km (180 miles) before he was found taking a nap by rangers and airlifted from the Nuweveld Mountains.
When he was found he was fitted with a tracking collar.
The second time he escaped, rescuers followed the signal from his collar to find him high up in the mountains in Western Cape again.
He was tranquilised and airlifted by helicopter, an operation the park authorities captured on video.
He had been away for four days.
Sylvester the lion in a stretcher on 31 March 2016Image copyrightSAN Parks
Image captionSylvester has a tracking collar on so was tracked down by helicopters and tranquilised
LionessesImage copyrightSAN Parks
Image captionThe park authorities hope Sylvester will bond with these two females and establish himself as the resident pride male in his new home
Read more →

Video ya Boko Haram yaonesha wasichana wa Chibok

,
;

Video ya Boko Haram yaonesha wasichana wa Chibok


WasichanaImage copyrightAFP
Image captionWanachama wa vuguvugu la Bring Back Our Girls waliandamana mjini Lagos Jumatano kutetea kuachiliwa kwa wasichana hao
Kanda ya video iliyotumwa kwa maafisa wa serikali ya Nigeria kutoka kwa kundi la wapiganaji wa Boko Haram inaonesha baadhi ya wasichana waliotekwa eneo la Chibok wako hai.
Ni miaka miwili tangu kutekwa kwa wasichana 276 kutoka shule moja katika mji wa Chibok.
Ni wasichana 15 wanaoonekana kwenye kanda hiyo ya video ambayo inaaminika ilipigwa Siku ya Krismasi.
Video hiyo imepeperushwa hewani na shirika la utangazaji la marekani la CNN.
Maafisa wa Nigeria wamesema mashauriano kati ya serikali na wapiganaji hao wa Kiislamu yanaendelea lakini yatasalia kuwa siri kwa sababu za kiusalama na ili kuzuia wanaofanikisha wazungumzo hayo wasitambulike.
MamaImage copyrightAFP
Image captionMamake mmoja wa wasichana waliotekwa
Mwandishi wa BBC aliyeko Abuja anasema video hiyo imewapa matumaini baadhi ya raia wa Nigeria kwa sababu inaonesha baadhi ya wasichana wako hai.
Lakini baadhi wanasema hali kwamba ni wasichana wachache sana waliooneshwa kwenye video hiyo inaibua wasiwasi kuhusu hatima ya wasichana hao wengine walioonekana kwenye video hiyo.
Kanda hiyo ya video ndiyo ya kwanza kutolewa ikiwaonesha wasichana hao tangu mwezi Mei mwaka 2014.
Serikali ya Nigeria imekosolewa kwa kushindwa kuwakomboa wasichana hao.
Chibok
Image captionShule ya Chibok inapatikana jimbo la Borno
Kwa muda mrefu, kitambulisha mada #BringBackOurGirls (Turejeshee wasichana wetu) kilivuma sana mtandao wa Twitter.
Mke wa Rais wa Marekani Michelle Obama ni mmoja wa watu mashuhuri walioshiriki katika kampeni ya kupigania kukombolewa kwa wasichana hao.
Read more →